Trusted by millions of Kenyans
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

“Huyu mwendawazimu anakuja nini kwenye sherehe hizi?Anafikiri sherehe hizi ni za watu wenye kichaa kama yeye”a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (al.4)b) Eleza tamathali...

“Huyu mwendawazimu anakuja nini kwenye sherehe hizi?Anafikiri sherehe hizi ni za watu wenye kichaa kama yeye”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (al.4)
b) Eleza tamathali mbili zilizotumiwa katika dondoo hili. (al.4)
c) Thibitisha kuwa anayerejelewa ni mwendawazimu na vile vile si mwendawazimu. (al.12)

Answers


ESTHER
a) Mashaka alijiuliza
Katika uwanja wa uhuru kuadhimisha siku ya wazalendo
Alimrejelea matuko weye alikuwa amehudhuria sherehe hii. (4x1 =4)
b) Balagha – anafikiri sherehe hizi ni za watu wenye kichaa kama yeye?
ii) Kinaya – matuko weye si mwenda wazimu huku kwani alitambua uovu wa Nasuba Bora. 2x2 =4
c) Ni mwendawazimu kwa sababu
- Ni mzee aliyekua hana mke wala watoto.
- Alivaa kaptura juu ya suruali zote zikiwa mararu.
- Hakumiliki chochote na aliweza kulala popote.
- Hakuvaa viatu tangu atoke vitani Burma.
- Aliboboja maneno ovyo ovyo.
- Alipopewa chakula alikulakitoweo kasha akala chakula
- Alipenda kupiga kwata. 1x6 =6
ii) Matuko weye si mwendawazimu.
- Alifaulu kupanda jukwaa na kuchukua kipasa sauti
- Hotuba yake inadhihirisha anafahamu maovu wanayofanyiwa na utawala wa mtemi Nasaba Bora.
- Alifanya kazi za sulubu ili kujikimu maishani.
- Alisema kuwa alijua kuwa Amani na Imani huwakumuua kitoto uhuru.
- Analaumu askari kwa kumshika na kasha kumwachilia bila kumpeleka mahakamani.
- Anamtaka imani aoelewe na azae watoto watakao ikomboa Tomoko kutoka kwa mkoloni mweusi.

ESTHER STEVE answered the question on September 7, 2018 at 20:00

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions