Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Jadili mbinu tano za lugha zilizotumika na mwandishi katika hadithi ya samaki wa nchi za joto

      

Jadili mbinu tano za lugha zilizotumika na mwandishi katika hadithi ya samaki wa nchi za joto.

  

Answers


KELVIN
Kinaya
? Christine kujivuta kidogo mbali na Zac ilhali anamtaka.
? Wewe lazima u msichana mwerevu-Peter-ni kinyume.
? Mimi? Kwa nini? Christine Zac anapomwambia Peter alitaka wamtembelee Tankhill-kujifanya hataki ilhali anataka.
? Zac usiwe mpumbavu. Mimi sitakwenda-anataka kwenda.
? Christine kusomea sosholojia ilhali mwenendo wake ni wa kukengeuka.
? Kunyoosha mkono wake alioulegeza kimakusudi kumsalimu Peter-kama htaki ilhali anataka.
? Sauti ya mchuuzi aliyepaaza sauti akimsihi awanunulie watoto wake peremende na kumwambia, “shangazi wakumbuke watoto na waonee huruma”.-ukweli ni kuwa ametenda kitendo cha kikatili cha kuavya mimba.
? Christine kuavya mimba ilhali hana mtoto mwingine.
Utohozi
? Ofisi ya Peter
? Maprofasa-wahadhiri wa chuo kikuu
? Balbu-taa
? Jenereta-kwa Peter-lililojiwAsha umeme ulipopotea
? Wikendi
? Shati-aliyovaa Peter akielekea Nairobi
? Glasi
? Sahani mbili nyekundu za plastiki
? Springi za kitanda
? Kozi-taaluma
? Noti ya dola 100 yenye thamani ya shilingi 1,000,000
Tashbihi
? Peter kumuuliza Christine anasomea kozi gani kama mjomba mkarimu anavyomuuliza mpwa wake.
? Ulaini wa ngozi yake (peter) ulikuwa sawa na wangu.
? Peter aliniongoza katika chumba chake cha kulala kama kwamba hilo lilikuwa jambo la kawaida.
? Peter kuangalia noti bandia kama mwanasayansi aliyekuwa akifanya uchunguzi maabarani-umakini.
? Uhusiano wetu niliuona kama kitendo cha watoto kwenda shuleni-kulazimika/kutokuwa na budi.
? Mhindi alimtumbulia macho kama kwamba alikuwa mzuka-Peter akikagua noti bandia.
? Baada ya kujihisi salama niliingiwa na wazo la kuwa debe bovu-kumfahamisha Peter hali yake ya hedhi.
? Nilitembea barabarani kama mtembea usingizini hadi katika kituo cha matatu-akitoka kwa Peter ofisini baada ya kumwambia aliavya mimba.
? Nikiwa na shahada ningekuwa kama ng’ombe wa kizungu-utamaaushi-hata akisoma, hakuna kazi ,mishahara duni, mazingira mabaya-ofisi kuukuu zilizojengwa wakati wa ukoloni.
? Umati ulipasua kicheko nilichokisikia kama radi.
Mbinu rejeshi
? Christine alikuwa ameokoka wakati mmoja
? Kisa cha Jagtit alichoshuhudia Christine alipompa Peter noto ya dola banda aliyokuwa amepewa na mhindi mwenzake Sunja Patel.
? Christine kueleza jinsi urafiki wao na Peter ulivyoanza kupitia Zac anayefanya kazi katika kampuni yake.
? Zac kueleza Christine jinsi Peter alivyoenda ‘Sailing Club’ na msichana mwingine.
? Kufahamishwa kuwa siku nyingi za Ijumaa jioni, Christine alikuwa anaondoka chuoni na kwenda kumtembelea Peter.
Jazanda/ Sitiari
? Anwani Samaki wan chi za Joto ni Jazanda.
? Samaki waliowala wale asili ni ukoloni mamboleo.
? Ndoto ya Dorothy kuhusu Christine ambapo aliota siku moja Christine alikuwa akipewa sumu na wazungu-akiharibiwa maisha.
? Huu ulikuwa msalaba wangu-mimba ni wajibu Christine pekee kwani hawakupanga na Peter kupata mtoto.
Sadfa
? Kukutana kwa Christine na Peter kupitia Zac wanayesoma naye Makerere na anayefanya kazi katika kampuni ya Peter.
? Christine kuwa kwa Peter kunasadifiana na Jagtit kumtembelea Peter kumuuzia dola. Uzungumzi nafsia
? Wewe baradhuli, kwa nini hukusema jambo lolote la maana- Christine akitoka kwa Zac akijisuta kwa kutochukua fursa kuanzisha urafiki na Peter.
? Nikweli Peter alinitaka?-Christine kujiuliza kimoyomoyo.
? Kwani Zac alifikiria sikumjua Peter vyema?-anapoambiwa walienda sailing club na msichana mwingine.
Kuchanganya ndimi
? ‘Penguin Classics’-vitabu vilivyokuwa juu ya dawati ya Zac.
? ‘Hey man’-kasumba ya Zac kuiga Waafrika weusi.
? ‘Half London’-wazungu wanakotafuta makahaba.
Takriri
? Najihisi mlevi, mlevi saana-na-Miriam.
? Hapana, hapana haiwezi kuwa bandia-jagtit kwa peter -kutoamini noti ni bandia.
Kicheko/tashtiti
? Christine kucheka akimwambia Peter kuhusu ndoto ya Dorothy.
? Peter kucheka anapoambiwa ndoto ya Dorothy na Christine.
? Umati ulipasua kicheko nilichokisikia kama radi.
Chuku
? Jagtit alipigwa na butwaa asiweze kuhoji kitendo cha Peter-kurarua noto bandia.
? Umati ulipasua kicheko nilichokisikia kama radi-baada ya kumsikia kijana aliyempaazia Peter Sauti kuwa angeambukizwa ukimwi na Christine.
? Kuwepo Entebbe Sailing Club kungemfanya awe mweusi zaidi-wengi ni wazungu.
Kejeli
? Kicheko ni kejeli kwa mtu kwa kutenda kitendo cha kijinga.
? Christine kusema akiwa na shahada angekuwa kama ng’ombe wa kizungu-elimu isingeboresha maisha yake.
? Christine anasikia sauti ya kejeli katika kicheko cha Peter anapomwambia ndoto kikisema watu weusi ni wajinga na washirikina wakubwa.
? Kijana anayempaazia Peter sauti akimkejeli Christine akisema kuwa angemwambukiza akimwi na alivyokondeana.

kalvinspartan answered the question on August 15, 2018 at 12:39


Next: Onyesha matumizi ya balagha katika hadithi fupi samaki wa nchi za joto
Previous: Onyesha ufaafu wa mada "damu nyeusi"

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions