Get premium membership and access revision papers, questions with answers as well as video lessons.

Kisumu District Mock- Kiswahili Paper 2 Question Paper

Kisumu District Mock- Kiswahili Paper 2 

Course:Secondary Level

Institution: Mock question papers

Exam Year:2007



JINA: ……………………………………………………………………... NAMBARI ….…………
SHULE:………………………………………………………………………………………………….
KISWAHILI
KARATASI YA PILI
LUGHA
JULAI/AGOSTI 2007
MUDA: SAA 2 ½
JARIBIO LA TATHMINI YA PAMOJA WILAYA YA
KISUMU 2007
HATI YA KUHITIMU KISOMO CHA SEKONDARI
KISWAHILI
KARATASI YA PILI
LUGHA
JULAI / AGOSTI 2007
MUDA: SAA 2 ½
MAAGIZO KWA MTAHINIWA
 Jibu maswali yote.
 Majibu yako yaandikwe katika nafasi zilizoachwa katika kijitabu hiki cha maswali
UFAHAMU (ALAMA 15)
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
1. Hadhari ubaraguzi, _mke ni fingo la nyumba,
Sijitiye ubazazi, kila kitu ukafumba,
Utamkausha ngozi, mke ni kama mgomba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
2. Simtiye simangizi, pa kheri kutia miba,
Mke akawa hawezi, chakula tabu kushiba,
Mke ni kama mdizi, huhitajia rutuba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
3. Usimianye kitwazi, mizigo yako kubeba,
Ukamkausha ngozi, nene akawa jembamba,
Mke siyo mpagazi, au nokoa wa shamba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
4. Mpe mema maikazi, mema ya ambao kwamba,
Na awe ndiye mlezi, kilicho katika nyumba,
Siyo wcnde matembezi, umwache kinywa cha fumba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
5. Mfanye ukimuenzi, mke mfanye suhuba,
Na kumpa maongezi, mazuri katika nyumba,
Awe ni msumlizi, wa furaha si msiba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
6. Mfanye ndugu mpenzi, mfanye kwako ni tiba,
Nenda naye matembezi, kama pesa na mkoba,
Mfanye awe hirizi, au cha lulu kikuba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
7. Muwekee matumizi, sanaa zisiwe haba,
Jitume ufanye kazi, mke apate kushiba
Na ikifikia mwezi, apate cha kujipamba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
8. Umpe mema malezi, atuwe katika nyumba,
Awe nao vijakazi, na vitwana kumpamba,
Msabiliye ghawazi, atumiye kujiramba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
9. Kumchezea maizi, mtunze mfano shamba,
Mpambe kwa vidarizi, vya dhahabu kumpamba,
Na kama hivyo huwezi, mpambe japo vya shaba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
10. Nafupiza beti hizi, ndugu kwenu nawaomba,
Nawaomba wasikizi, wake muwape vilemba,
Dahari wawe azizi, moyoni wawe na hiba,
Mke ni fingo la nyumba, hadhari kumchezea.
Maswali. (alama 15)
1. Andika kichwa mwafaka cha shairi hili.
(alama 1)
……………………………………………………………………………………………………
2. Kwa kusema, ‘Mke ni fingo la nyumba’ mwandishi ana maana gani? (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
3. Kulingana na ubeti wa 3 na 5, mshairi anapendekeza mme aishi vipi na mkewe? (alama 3)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
4. ‘Mke ni nguo, mgomba kupalilia.’ Kwa kurejelea shairi hili, thibitisha kauli hii. (alama 4)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
5. Mke anawezaje kuwa tiba kwa mme? (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
6. Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivotumiwa katika shairi. (alama 3)
(i) Ubazazi
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
(ii) Simangizi
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
(iii) Mdizi
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
UFUPISHO
Tukichungua maisha ya vijana wa leo kwa jicho la kuona ndani sana, tutavumbua mambo mengi ya kushtusha. Lengo kuu la vijana hawa ni kupata kazi zenye chungu ya pesa, nyumba nzuri, tofauti na za kiafrika, magari mazuri yenye nguvu na mbio na mitambo mingine yenye kuwawezesha kutenda
mambo bila ya kukipurukisha kiungo chochote. Wao wataka shida ziwe ng’ambo ya uoni wao.
Mapenzi, yaliyoitwa umoja wa masikilizano ya kinyumba na kilimwengu sasa yamegeuzwa na vijana wa leo yaitwe uhayawani, dosari, kutosikilizana na ari ya kujiokoa nafsi zao zinazoteketea. Mara nyingi watoto wa kike waolewapo na iwapo wanafanya kazi kama mabwana zao, hao huwa kwa thuluthi kubwa ya maisha yao, wanajitegemea na kujiona kama wanaishi na mabwana zao kama ada tu, bali wana uhuru wa kutenda vyovyote vile wapendavyo.
Iwapo wake wa namna hii watakemewa, hutisha kuwa watawaacha mabwana au kila mmoja wao awe
na sehemu ya utawala katika nyumba zao maana kila mmoja anacho mwenziwe alichonacho. Bwana
ana pesa -bibi anazo, bwana ana gari- bibi analo, bwana ana digrii- bibi anazo nyingi na kadhalika.
Vijana wa kiume wawapo hawana ari ya kuoa, wazazi wenye wana wa kike hupata hasara kubwa
kama mfalme kuondolewa jeshi lake la adui wake: wasichana walioachiwa kazi mahsusi kuzitenda au wasichana shuleni, waingiapo katika zogo na zahama za vijana wa leo za masinema, magoma ya mchana na usiku na mikutano isiyokwisha mara hushtukia wameingia katika njia ya umama na mababa hawajulikani. Iwapo baba anajulikana, thuluthi tisaini na tisa kwa mia ya wazazi wa namna hii, hukataa katakata kuwa wahusika na mamba za namna hii.
Yote haya yanasababishwa na mtambo mkubwa wa uhalifu- pesa. Wanawali wengi hutoa jasho kwa
kufukuza pesa wazionazo upeoni mwa macho yao. Wasichana hawa huwaghilibu wavulana ambao
wamezikokota katika matope.
Vijana wengine huwa radhi kabisa kupoteza maisha kwa kuingilia uhalifu ili wapate uti wa
kuwawezasha kustarehe na wasichana wa majumba yauziwayo pombe na wale wanyonyaji wazururao
katika barabara pana za miji mikubwa nchini ya taa zenye rangi. Wasichana hujiharibu wajihi wao wakawa kama vinyago vya uzazi wa kale.
MASWALI
(a) Kulingana na aya tatu za kwanza, vijana wa siku hizi kupendelea kuishi maisha ya aina gani?
(maneno 70 – 80 ) (alama 6)
Nakala chafu
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
Nakala safi.
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
(b) Maisha ya vijana yana madhara gain kwa vijana wasipokuwa na tahadhari ya maisha.
(maneno 90 – 100) (alama 6)
Nakala chafu
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
Nakala safi.
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
MATUMIZI YA LUGHA. (alama 40)
A. Bainisha kisha utaje aina za vielezi katika sentensi zifuatazo!
(i) Mgonjwa alitembea kivivu halafu akagonga mlango ngo! ngo! ngo! (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
(ii) Msafara wa magari ulielekea Nairobi jana usiku. (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
B. Tumia kielelezo cha jedwali kuchanganua sentensi hii.
Mwalimu kijana alitufundisha Kiswahili jana asubuhi. (alama 3)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
C. Bainisha aina ya kirai katika sentensi ifuatayo.
Mwalimu amempiga (alama 1)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
D. Tumia T, Ts na t kubainisha vitenzi katika sentensi zifuatazo. (alama 3)
(i) Baba alikuwa angali analala
……………………………………………………………………………………………………
(ii) Oliech angali mchezaji.
……………………………………………………………………………………………………
(iii) Wazazi wamekwisha fika shuleni
……………………………………………………………………………………………………
E. Tofautisha kati ya sentensi zifuatazo kasha utunge sentensi moja moja
(i) Sentensi sahili (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
(ii) Sentensi ambatano (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
(iii) Sentensi changamano. (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
F. Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli zilizotajwa. (alama 2)
Tendea Tendesha
- fa --------------------- ----------------------------
- la --------------------- -----------------------------
G. Geuza sentensi ifuatayo katika usemi halisi:
Mgeni alisema ya kwamba angerudi siku iliyofuata. (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
H. Badilisha sentensi ifuatayo katika hali ya ukubwa na udogo
Mzee yule alikalia ngoma kama kiti
(i) Ukubwa (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
(ii) Udogo (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
I. Tumia viambishi virejeshi katika sentensi ukitumia maneno yafuatayo
(i) Kamata (alama 1)
……………………………………………………………………………………………………
(ii) Ogopa (alama 1)
……………………………………………………………………………………………………
J. Andika upya sentensi zifuatazo kwa kufuata maagizo yaliyomo mabanoni.
(i) Mama alipoenda tulilia na kulala. (andika kinyume) (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
(ii) Nilikaa nyumbani ndiposa ulinipata. (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
K. Tambulisha aina za shamirisho katika sentensi. (alama 3)
Mtoto alimlimia mamake shamba kwa jembe
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
L. Eleza maana tatu tofauti za sentensi hii.
Onyango alimpigia mtoto mpira. (alama 3)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
M. Eleza matumizi yoyote matatu ya ‘NA’ na kasha utunge sentensi kuonyesha matumizi hayo.
(alama 3)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
ISIMU JAMII (alama 10)
Soma mazungumzo yafuatayo kasha ujibu maswali.
A: Hepu nikuambieko mwana!
B: Eeh! Dakua nisikieko. Dadangu!
A: Tuniani kuna watu na fiatu
B: Mbona umependaga kuniambia mafumbo?
A: Wacha nikuelezeko! Jumamosi kwa kina wafulana nikampata mamake. Sichui alidhani
mimi hushindanga njaa kwetu. Gumtu gulinina gukafunga mlango ndi! Gukaanza
kuniangalia kupitia dirisha.
B: Pole! Sichui wengine hufanyanga wenzao ache- Mwache tu, siku moja Mulungu
atakapatieko kipigo cha mwaka.
A: Mwana, wacha niendeko salon nikatengenezeko nywele zangu. Tuonane kesho
MASWALI
1. Eleza muktadha wa mazungumzo haya. (alama 4)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
2. Ni kipengele kipi cha lugha kinadhihirika katika mazungumzo haya? Fafanua. (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
3. Kuna mambo kadhaa yanayoweza kuathiri matumizi ya lugha kwa ujumla katika jamii. Taja
na ueleze kwa ufupi mambo yoyote manne. (alama 4)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………






More Question Papers


Popular Exams



Return to Question Papers